

Anajiita Mzee wa Mahaba kutoka Manzabay,Cassim Mganga akiwaimbisha mashabiki wake kwa shangwe huku mayowe yakitawala kila kona ya uwanja wa Kambarage usiku huu ndani wakati tamasha la Serengeti fiesta likiendelea kurindima usiku huu.



Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,Rich Mavoko akiimba jukwaani usiku huu sambamba na madensa wake (hawapo pichani).


Mashabiki wake wanamuita Kinga Zilla kutoka Sala Sala,lakini pia jina la Godzilla limemuongeza umaarufu kwa mashabiki wake kutokana na umahiri wake wa kushusha mistari ya hip hop mikavu mikavu,kama aonekavyo jukwaani akiwaimbisha mashabiki wake ndani ya uwanja wa Kambarage usiku huu.


Baadhi ya wakazi wa mji wa Shinyanga wakiwa wamejitokeza kwa wingi usiku huu kwenye uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga,ambapo tamasha la Serengeti Fiesta 2013 likiendelea kufanyika.

Mwanadada Linah akiimba sambamba na shabiki wake jukwaani usiku huu wakati tamasha la serengeti fiesta likiendelea ndani ya uwanja wa Kambarage,mkoani Shinyanga usiku.

Baadhi ya Wadau wakubwa na wadhamini wa Tamasha la Serengeti Fiesta 2013,kutoka kampuni ya Serengeti Breweries,Octavian,Bahati pamoja na mdau wao,wakiwa katika picha ya pozi usiku huu ndani ya uwanja wa Kambarage,mkoani Shinyanga

Mwanadada ambaye kwa sasa ameonekana akifanya vyema kwenye jukwaa la Serengeti fiesta 2013,Neylee akiwaimbisha mashaniki wake (hawapo pichani).

Anajiita Jita Man kutoka jijini Mwanza akitumbuiza jukwaani usiku huu.

Dj Zero kutoka Clouds FM akiburuza mangoma usiku huu.


Mwanadada Shilole na madensa wake wakilishambulia jukwaa vilivyo usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti fiesta 2013,ndani ya uwanja wa Kambarage.mkoani Shinyanga.

















No comments:
Post a Comment