Pages

Monday, June 30, 2014

MISS SHINYANGA 2014 APATIKANA,TAZAMA PICHA KIBAO HAPA



Hatimaye mkoa wa Shinyanga umepata mrembo(Redd's Miss Shinyanga 2014),mrembo huyu si mwingine bali ni  Nicole Franklyn Sarakikya(katikati) aliyekuwa akiwakilisha wilaya ya Kishapu,lakini pia Miss Kishapu 2014.Mashindano ya kumpata mrembo wa mkoa wa Shinyanga yamefanyika Juni 28,2014 mjini Kahama katika ukumbi wa NSSF yakiwa yameandaliwa na Asela Promotion ikisimamiwa na bi Asela Magaka.Waliosimama ni warembo ambao waliingia katika top 5.

Washiriki  walioingia 5 bora katika  shindano la Redd's Miss Shinyanga 2014 lililofanyika usiku wa kuamkia leo mjini Kahama ambapo jumla ya warembo 20 kutoka maeneo mbalimbali kutoka mkoa wa Shinyanga walikuwa wakiwania taji hilo.Kati ya hao 5 bora mmoja aliibuka mshindi wa kwanza
Mshindi wa kwanza katika kinyang'anyiro hicho ni bi Nicole Franklyn Sarakikya kutoka wilaya ya Kishapu,mshindi wa pili ni Mary Emmanuel kutoka Ushetu,mshindi wa tatu ni Rachel Judica kutoka Shinyanga vijijini ,mshindi wa nne ni  Nyangi Warioba kutoka Msalala,  na mshindi wa 5 Neema Kakimpa kutoka wilaya ya Kahama
Mshindi wa taji la Redd's Miss Shinyanga 2014 bi Nicole Franklyn Sarakikya kutoka wilaya ya Kishapu.Katika mashindano hayo ya kupata mrembo wa mkoa wa Shinyanga yaliyoandaliwa na Asela Promotions,mshindi wa kwanza ameibuka na kitita cha Shilingi la 500,000/= na Laptop moja,mshindi wa pili shilingi 350,000/= mshindi wa tatu shilingi 250,000/=,mshindi wa 4 shilingi 150,000/= na mshindi wa tano shilingi 150,000/= huku washiriki wengine waliosalia kati ya 20 wakipata shilingi 100,000/= kila mmoja.
Katikati ni mshindi wa kwanza shindano la Redd's Miss Shinyanga 2014 Nicole Sarakikya,kushoto ni mshindi wa pili ni Mary Emmanuel,kulia ni mshindi namba tatu  ni Rachel Judica ambao watashiriki katika shindano la kutafuta mrembo wa kanda ya ziwa lililoandaliwa na Flora Salon

Saturday, June 21, 2014

AMANI WA KENYA NA MO MUSIC KUKAMUA MISS SHINYANGA 2014‏




Warembo hao wakifanya mazoezi katika ukumbi wa Ihesa Hotel & Resort Ltd ya mjini Kahama.
Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Mo Music akiwa katika pozi siku ya jana Global Tv Online.
Mwanamuziki, Amani wa Kenya.
Na Mwandishi Wetu (Ali Lityawi),
Kahama,
Juni 15, 2014
WAREMBO 20 wanatarajia kupanda jukwaani Juni 28, mwaka huu ndani ya ukumbi wa Shirika la Hifadhi ya Jamii ( NSSF) wilayani Kahama kuwania Taji la Redd's Miss Shinyanga 2014.

Kwa mujibu wa waratibu, Kampuni ya Asela Promotion, shindano hilo litashirikisha Warembo kutoka katika Wilaya sita za Mkoa wa Shinyanga ambazo ni Kishapu, Kahama, Shinyanga Mjini, Msalala Shinyanga Vijijini na Ushetu.
Mratibu wa shindano hilo, Asela Magaka alisema mwaka huu anatarajia Redd's Miss Tanzania 2014 atatoka mkoa wa Shinyanga kutokana na warembo waliopo kambini kuwa na vigezo, mvuto mkubwa na viwango vinavyofaa kunyakua taji hilo.
Magaka aliwataja warembo hao kuwa ni Aisha Ally, Grace Lyimo, Pendo Maxmillian, Mary Bugingo, Irine Hamedi, Neema Kakimpa,Jacquline Robert, Nilam Siraji, Grace Kimaro, Sophia Mhina, Jacline Kimambo, Rose Shunda na Lawrancea Mathew.
Aliwataja Warembo wengine kuwa ni Rachel Mushi, Hadija Nyanda, Nyangi Warioba, Rockie Bangili,Jacline Jacksoni, Lukia Samili na Nicole Sarakikya hivyo kuwataka mashabiki na wapenzi kujitokeza kwa wingi kushuhudia nani anatwaa taji la Mrembo wa Mkoa wa Shinyanga.
“Warembo tayari wameanza mazoezi katika ukumbi wa Ihesa Hotel & Resort Ltd ya mjini Kahama na washindi watatu watawakilisha mkoa wa Shinyanga katika michuano ya Kanda” Alisema Asela Magaka.
Aidha aliwataja wadhamini wa Shindano hilo kuwa ni SSCN TV ya Mjini Kahama, Nonema Investiment, Trixie Social Media Market, Nyamizi Secretarial Service, Royal Supermarket, NSSF, Coca Cola, Redd's na Global Publishers.
Wengine ni pamoja na Clouds FM, Three Jays’s Inverstment, CXC Africa, Williamson Diamond, Saluti5, Ihesa Hotel, Kahama Commonity Health Dispensary, Tulliz Fashion, Ngeleja Gold Mine, Kahama Motel, Charitk Pub, Glory Pads na Barrick Buzwagi.

Tuesday, April 29, 2014

FURSA: MAFUNZO YA KUPIGA ALA ZA MUZIKI KUANZA TENA MWEZI MEI‏

 Baadhi ya wanafunzi wakiwa kwenye mazoezi

Action Music Tanzania (AMTz) inatangaza fursa kwa watu wote kujiunga na mafunzo ya kupiga ala za muziki yanayoanza tarehe 3/5/2014, lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wanamuziki wa kupiga ala na kufanya maonesho kwa weledi na utaalamu zaidi.
Baadhi ya wanafunzi wakiwa darasani

Mafunzo yanayotolewa ni pamoja na upigaji wa ala za muziki zikiwemo gita, kinanda, tarumbeta, saxophone, konga, drum set, na upigaji wa ngoma za asili. Pia yatatolewa mafunzo ya ‘body percussion’ yaani matumizi ya mwili katika kutengeneza midundo ya muziki.

Mafunzo hayo yanafanyika kwenye ofisi za AMTZ zilizopo maeneo ya Mwenge mtaa wa Umoja, nyuma ya magorofa ya jeshi na kwenye Idara ya Sanaa na Sanaa za Maonesho Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo ili kujiunga na mafunzo haya wasiliana nao kwa simu namba 0686928828/0653075791 ili kupata fomu za kujiunga na mafunzo.

  

         


Sunday, February 2, 2014

TAZAMA SHOW YA OMMY DIMPOZ NDANI YA KAHAMA SHINYANGA YAFUNIKA MBAYAAAAA




IMG-20140201-WA0018
IMG-20140201-WA0000


Ommy Dimpoz kupitia kampuni yake ya Poz kwa Poz Entertainment ameendelea kujiimarisha kwa kuandaa show zake mwenyewe ambapo jana alitumbuiza wilayani Kahama, Shinyanga na kuujaza ukumbi wa Social.
Ommy ameiambia Bongo5 kuwa kile anachokifanya sasa kinaweza kuwa changamoto kwa wasanii wengine nchini kuanza kujiandalia show zao wenyewe na sio kusubiri hadi wapigiwe simu na mapromoter. Leo atakuwa na show nyingine aliyoaindaa mjini Geita kwenye ukumbi wa Ambassador na anasindikizwa na mshindi wa EBSS, 2012, Walter Chilambo.
Hizi ni picha za show ya Kahama.
IMG-20140201-WA0001
IMG-20140201-WA0002


IMG-20140201-WA0003
IMG-20140201-WA0005


IMG-20140201-WA0006
IMG-20140201-WA0007


IMG-20140201-WA0008
IMG-20140201-WA0009


IMG-20140201-WA0010
IMG-20140201-WA0011


IMG-20140201-WA0012
IMG-20140201-WA0014

IMG-20140201-WA0015
IMG-20140201-WA0017

Sunday, October 27, 2013

Cheki Burudani za Serengeti Fiesta 2013 Ndani Ya Uwanja Wa Kambarage Mjini Shinyanga





Anajiita Mzee wa Mahaba kutoka Manzabay,Cassim Mganga akiwaimbisha mashabiki wake kwa shangwe huku mayowe yakitawala kila kona ya uwanja wa Kambarage usiku huu ndani wakati tamasha la Serengeti fiesta likiendelea kurindima usiku huu.
Mtoto wa Mama Saidi a.k.a Cheke akiimba kwa hisi jukwaani.

Msanii wa Bongofleva Ney wa Mitego akiwaimbisha mashabiki wake.

Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,Rich Mavoko akiimba jukwaani usiku huu sambamba na madensa wake (hawapo pichani).
Tamasha la Serengeti fiesta 2013 likiendelea usiku huu.

Mashabiki wake wanamuita Kinga Zilla kutoka Sala Sala,lakini pia jina la Godzilla limemuongeza umaarufu kwa mashabiki wake kutokana na umahiri wake wa kushusha mistari ya hip hop mikavu mikavu,kama aonekavyo jukwaani akiwaimbisha mashabiki wake ndani ya uwanja wa Kambarage usiku huu.


Baadhi ya wakazi wa mji wa Shinyanga wakiwa wamejitokeza kwa wingi usiku huu kwenye uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga,ambapo tamasha la Serengeti Fiesta 2013 likiendelea kufanyika.

Mwanadada Linah akiimba sambamba na shabiki wake jukwaani usiku huu wakati tamasha la serengeti fiesta likiendelea ndani ya uwanja wa Kambarage,mkoani Shinyanga usiku.

Baadhi ya Wadau wakubwa na wadhamini wa Tamasha la Serengeti Fiesta 2013,kutoka kampuni ya Serengeti Breweries,Octavian,Bahati pamoja na mdau wao,wakiwa katika picha ya pozi usiku huu ndani ya uwanja wa Kambarage,mkoani Shinyanga

Mwanadada ambaye kwa sasa ameonekana akifanya vyema kwenye jukwaa la Serengeti fiesta 2013,Neylee akiwaimbisha mashaniki wake (hawapo pichani).

Anajiita Jita Man kutoka jijini Mwanza akitumbuiza jukwaani usiku huu.

Dj Zero kutoka Clouds FM akiburuza mangoma usiku huu.


Mwanadada Shilole na madensa wake wakilishambulia jukwaa vilivyo usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti fiesta 2013,ndani ya uwanja wa Kambarage.mkoani Shinyanga.

Masbabiki kibao waliojitokeza kwenye tamasha la serengeti fiesta 2013,usiku wakifuatilia na kushangweka vilivyo mbele ya jukwaa la fiesta.
mashabiki wakifuatilia
Kutoka Wanaume TMK,wakiongozwa Mh Temba na Chege kwa pamoja wakilishambulia jukwaa la Serengeti fiesta usiku huu ndani ya uwanja wa kambarage mjini Shinyanga.
Weusi wakitumbuiza jukwaani usiku huu.
Shabiki akifurahi jamboo.
Kundi la Wanaume TMK-Halisi likiongozwa na Sir Juma Nature wakilishambulia jukwaa la Serengeti Fiesta ndani ya uwanja wa Kambaraje,mjini Shinyanga.